• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI ZIARA YA ALAT MKOA WA RUVUMA WALIPOTEMBELEA MKOA WA KATAVI

Tarehe ya kuwekwa: July 6th, 2024

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za  Mikoa  Tanzania (ALAT) Mkoa wa Ruvuma Kelvin Mapunda amewaongoza wajumbe wa ALAT Mkoa wa Ruvuma na kuwasili katika Mkoa wa KATAVI katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  kwa lengo la kujifunza namna ya uendeshaji na usimamizi wa Biashara ya Kaboni.

Biashara ya  kaboni  Wilaya ya Tanganyika  imelenga  kuhifadhi  Mazingira  (Misitu),  kulinda na Kuhifadhi Bioanuai zote muhimu na zilizo hatarini kutoweka Duniani (Sokwe mtu), kutunza vyanzo vya maji na Wanyamapori wengineo na kuwaletea Maendeleo endelevu kwa jamii inayozunguka au kuzungukwa na Misitu katika dhima ya kupambana na Mabadiliko ya tabia nchi na madhara yake.

 Mradi huo  umelenga kuziwezesha jamii kufanya shughuli za maendeleo za vijiji kupitia mapato yatokanayo na kuuza hewa ya kaboni baada ya kuhifadhi Misitu yao kwa kuzuia uharibifu au ukataji miti katika maeneo ya vijiji yaliyohifadhiwa na kusimamiwa kisheria na wanajamii wenyewe sambamba na  kuboresha huduma kwa jamii pamoja na kuhusisha jamii  katika  uhifadhi na  kunufaika  moja kwa moja na faida za uhifadhi.

Hayo yamejiri wakati wa ziara ya Jumuiya ya Tawala za Mikoa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Ruvuma walipotembelea Mkoa wa Katavi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika iliyofanyika tarehe 03 Julai 2024 kwa lengo la kujifunza namna ya uendeshaji wa Biashara ya Kaboni.

Akizungumza mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma  Kelvin Mapunda  amewataka  wajumbe wa kamati ya ALAT Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanajifunza  mafunzo hayo  kwa umakini na kuhakikisha  wanakwenda  kutekeleza  kwenye  Halmashauri  sambamba na kuhusisha  jamii katika uhifadhi na kunufaika na uhifadhi.

Katibu  Tawala Msaidizi Mkoa wa Katavi  Neemia James  alisema  “Biashara kaboni ilianza mwaka 2018 ukiendeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, Taasisi ya CARBON TANZANIA kwa kushirikiana na Mradi wa TUUNGANE kwa afya na Mazingira bora katika Wilaya ya Tanganyika ambapo  Biashara hiyo  inatekelezwa  katika Vijiji nane (8) ambavyo ni Lugonesi, Mwese, Lwega, Bujombe, Kapanga, Katuma, Mpembe na Kijiji cha Kagunga yenye jumla ya  ukubwa wa Hekta 216,944 za ardhi katika vijiji vyote vyenye  jumla ya wakazi 34,242 wanaofaidika na mradi huo.”

Alisema ili uweze kufanikisha kuanzisha biashara ya kaboni inahitaji kutekeleza hatua zifuatazo ikiwemo na Vijiji kuwa na mpango wa matumizi bora ya Ardhi,  uwepo wa msitu uliotengwa kwenye mpango wa matumizi ya ardhi, Uwepo wa tangazo la Serikali (GN), kwa misitu  ya Serikali kuu na Halmashauri,  Misitu kuwa na mipango ya usimamizi (forest Management plan) , hii inaweza kuandaliwa mchakato ukiwa unaendelea kuwa na uthibitisho wa umiliki wa msitu, kuwa na eneo la kutosha (kubwa ) angalau hekta 50, Msitu usiwe wa uvunaji na ulindwe usiharibiwe.

Wakieleza  faida zinazopatikana kutokana na mradi huo ni amoja na Misitu iliyotengwa na vijiji hufyonza hewa chafu zinazozalishwa kutoka viwandani ambapo  vyombo vya usafiri na wanyama hasa binadamu  huchangia katika kupunguza kiwango cha kaboni  kwenye anga pamoja na Misitu iliyohifadhiwa husaidia kutunza vyanzo vya maji vinavyohakikisha upatikanaji wa maji na mvua za uhakika.

Aidha Faida nyingine ni mgawanyo wa fedha Kiasi cha  Shilingi bilioni nne (4,276,000,000) kilichopatikana katika awamu ya sita 6  na saba 7 ambacho kilikabidhiwa katika Vijiji nane (08) nufaika wa biashara ya kaboni  ambapo  Kati ya fedha hizo, Halmashauri ya Wilaya ilipokea Shs.427,600,000 sawa na 10% na Vijiji  nufaika Shs. 3,600,000,000 sawa na 90% pia Uchangiaji mapato katika Halmashauri kupitia mapato ya ndani ambapo tangu mradi umeanzishwa Halmashauri imekusanya zaidi ya shilingi milioni mia nane  ishirini na tano laki sita (825,600,000) sawa 10% ya mapato.

Aliongeza kuwa faida nyingine ni utoaji  wa ajira kwa jamii ambapo jumla ya vijana  (200) wameajiriwa kama askari walinzi wa misitu ya vijiji  kwa ajira hiyo hulipwa posho ya shilingi laki tatu (300,000) kila mmoja kwa kila mwezi, Ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Katuma na ujenzi wa Zahanati 6 katika vijiji vya Lugonesi, Kapanga, Mpembe , katuma  Kagunga na lwega ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, pamoja na Utoaji wa Bima za afya kwa wakazi wote waishio kwenye vijiji vya kaboni ambapo hadi Juni februari 2023 kaya 4400 sawa na watu 26273 walipatiwa bima za afya.

Miradi mingine ni  Ujenzi wa vyumba vya madarasa 52 kwenye vijiji 8 vya Kaboni na katika shule 1, Ujenzi wa jengo la Utawala katika Shule ya Sekondari Mwese, Utoaji chakula kwa wanafunzi shule za Msingi, Ajira za mkataba kwa Walimu  22 katika shule za msingi ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu, ambapo walimu hao hulipwa Shs. 300,000,  pia ujenzi wa nyumba za Watendaji wa kijiji cha  Lwega,  Utoaji posho za madaraka kama motisha kwa Wenyeviti na Watendaji wa vijiji ambao hulipwa Shs.300,000 kwa Wenyeviti na Shs.200,000 kwa Watendaji wa vijiji kila mwezi. “Alibainisha”

Wakizungumza na chanzo hiki cha habari baadhi ya wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Ruvuma, wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kuanzisha mradi wa Kaboni ambao unanufaisha jamii, pia unaongeza mapato katika Halmashauri.

IMEANDALIWA  NA; 

AMINA PILLY.

MWANDISHI ALAT RUVUMA.                                                                                               

 



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa