• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI KIKAO CHA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM - SONGEA MJINI.

Tarehe ya kuwekwa: September 15th, 2022

IBARA ya 76 ya Katiba ya Chama Cha Mapinduzi katika  Ibara ndogo ya 4 Ukurasa  namba 76 wa katiba umetamka Kazi na Majukumu ya Halmashauri  Kuu ya chama ikiwemo  na Kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo, kusimamia na kuhakikisha Ilani ya CCM inatekelezwa.

Aidha, mabadiliko ya katiba mpya imeongezwa majukumu ya Halmashauri kuu ya Kata ambayo imeeleza katika Ibara ya 50 katika Ibara ndogo ya 4 Ukurasa namba 43  umewataka kutekeleza majukumu ngazi ya Kata, Wilaya hadi Mkoa, hata hivyo utekelezaji wa maagizo hayo unatakiwa kutekelezwa kuanzia sasa.

Katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi  Mwenyekiti wa CCM Songea Mjini Hamisi Abdallah Ally ameongoza kikao maalmu cha Utekelezaji wa Ilani  ambacho kilihudhuriwa na wajumbe wa Halmshauri kuu ngazi ya Kata  kilichofanyika tarehe 14 Septemba 2022 katika Ukumbi wa CCM tawi la Songea Mjini kwa lengo la kupokea taarifa ya utekelezaji kutoka kwa Mkuu wa Wilaya.

Hamisi amewataka viongozi wa vyama vya siasa wasiwe sehemu ya walalamikaji katika maeneo yao bali wawe viongozi  wafuatiliaji wa shughuli zote zinazofanywa na Serikali ili kuondoa malalamiko kwa wananchi wanaowaongoza.

 Aliongeza kuwa kila kiongozi anapaswa kutambua miradi yote inayotekelezwa na Halmashauri katika maeneo wanayoishi na kujijengea tabia ya kufanya ziara mara kwa mara kwa lengo la kukagua  mradi na  kufahamu muda wa kuanza kwa  mradi, ukomo wa utekelezwaji wa mradi na gharama za mradi husika ili waweze kuisemea Serikali kwa wananchi. Alisisitiza

Ametoa rai kwa wataalamu wa TARURA  kuchonga barabara chache  zenye viwango vinavyotakiwa kulingana na mpango na bajeti iliyowekwa na kuacha kuchonga barabara nyingi chini ya kiwango kwa ajili ya kuwanufaisha  viongozi wa vyama vya siasa kitendo ambacho kinaathiri miundombinu ya barabara na kusababisha malalamiko kwa wananchi.

Hamisi, amewataka wataalamu wa kilimo kutumia pikipiki zilizotolewa na Serikali kwa kuwatembelea wakulima mashambani pamoja na kufanya upimaji wa udongo ili wakulima waweze kulima kilimo chenye tija.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho alitumia fursa hiyo  kuwapongeza viongozi wote kwa kuchaguliwa katika chaguzi mbalimbali zilizofanyika hivi karibuni kuanzia ngazi ya Shina, Tawi, na Kata na kuwataka kila mmoja katika nafasi yake atekeleze wajibu wake.

Oddo alibainisha kuwa jambo muhimu katika chama cha mapinduzi ni kuendelea kudumisha Ushirikiano ndani ya chama, kuimarisha Chama kiuchumi, kisiasa, na kuendelea kujitegemea kwa kuanzisha miradi mipya au kuendeleza miradi iliyopo.

Akisoma taarifa hiyo Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 ni Kuhakikisha kwamba halmashauri zote nchini zinaendelea kutenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu kwa mujibu wa sheria ili kuwezesha vijana  na makundi mengine katika jamii zetu kupata mikopo isiyo na riba.

Pololet alisema kuwa Katika kutekeleza maelekezo ya Ilani kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ilifanikiwa kuhamisha fedha kutoka akaunti ya makusanyo kwenda kwenye akaunti ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kiasi cha tshs 356,700,000.00 hadi kufikia septemba, 2022 jumla ya tshs 250,000,000.00 kimetolewa kwenda kwenye akaunti ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu sawa na asilimia 70.08 ya lengo.

Alisema Mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia TASAF awamu ya III kipindi cha kwanza ulianza kutekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuanzia mwaka wa fedha 2015/2016, ambapo jumla ya mitaa 53 imenufaika na mpango huu, hadi sasa jumla ya kaya 5,618 zimenufaika na Mpango huu wa kunusuru kaya maskini.

kipindi cha mwezi Julai hadi septemba, 2022/2023 Halmashauri inaendelea na ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa na mabweni 2 katika shule ya Wasichana ya Songea na vyumba 3 vya madarasa na mabweni 2 katika shule ya wavulana Songea. Ujenzi wa miradi hii upo katika hatua mbalimbali, ambapo gharama za ujenzi wa miradi hii inayoendelea ni Tshs. 540,000,000.00

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa