• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZAIDI YA AINA YA DAWA 975 HUTOLEWA HUDUMA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA.

Tarehe ya kuwekwa: September 9th, 2020

Kauli hiyo imetamkwa na Afisa mwandamizi Idara ya Uanachama Mkoa wa Ruvuma Katondo Gideon katika kikao cha  Watumishi Sekta ya Elimu kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea leo 09.09.2020.

Katondo alisema MTBA ni taasisi ya Umma iliyoundwa kwa mujibu wa Sheria Na. 8 Sura Na. 395 TL 1999 na Utekelezaji wake ulianza Julai 2001 ambayo ni matokeo ya utekelezaji wa Sera ya mabadiliko katika Sekta ya Afya (1990s), kwa lengo la kutoa Bima ya Afya kwa makundi mbalimbali kwa wananchi, kujenga uwezo wa  kipato kwa vituo, kushirikisha sekta binafsi katika kuharakisha maendeleo katika sekta binafsi.

Alisema Mfuko wa Bima ya Afya  unamilikiwa na Serikali kwa 100% na unasimamiwa na Bodi ya Wakurugenzi inayojumuisha wadau muhimu Nchini. Dhana ya  Bima ya Afya imejengeka katika misingi ya mshikamano wa kijamii katika kuchangiana gharama za matibabu.

Alibainisha kuwa Mtumishi huchangia 6% ya mshahara wake wa mwezi kwa usawa kati ya mwajiri 3% na mwajiriwa 3% na kuwa na jumla ya  Wanufaika ni sita (6) na iwapo mume na mke ni wachangiaji idadi ya Wanufaika ni (10) ambao pia Wanufaika ni mwanachama mchangiaji, mwenza wake, watoto wa kuzaa au kuasili, wake/wakwe ikiwa pamoja na uwasilishaji wa nyaraka za uthibitisho. Alisistiza.

Aliongeza kuwa Katika kuongeza uwigo wa Wanachama wake, Mfuko umeanzisha huduma mpya ambayo ni Toto Afya Kadi  (Watoto wa ziada wanaweza jumuishwa  katika  utaratibu huu), Wanafunzi, Ushirika Afya (wakulima kupitia AMCOS), Madereva Bodaboda, Vifurushi vya bima (Najali, Wekeza na Timiza.

Alisema  huduma za matibabu hupatikana  popote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo ni zaidi ya vituo 8,022 vinavyotoa huduma za matibabu bila kujali hali ya afya au kiasi cha mchango pamoja na huduma za matibabu kwa mwanachama mstaafu na mwenza wake katika  maisha yao yote.

Katondo akitaja mafao yatolewayo na Mfuko wa Bima ya Afya nipamoja na  ada ya uandikishaji na ushauri wa tiba, huduma ya wagonjwa wa nje, huduma ya Dawa zaidi ya aina 975, huduma ya wagonjwa wa ndani,  huduma za Vipimo  mbalimbali,  huduma za matibabu ya kinywa, huduma za upasuaji wa aina zote (moyo, mifupa, mishipa ya fahamu etc).

Aidha, katika kikao hicho kuliibuka na malalamiko kutoka kwa Watumishi  hao wakilalamikia Mfuko wa Bima ya Afya kuwaondoa wanachama ambao wamefikia au kuzidi umri wa miaka 18 bila kujali kama ni wanafunzi wa shule. Naye Afisa mwandamizi wa Uanachama Mkoa wa Ruvuma Katondo Gideon alisema nanukuu  “ hiyo ni sheria ambayo ilishatungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwahiyo ipo kwenye utekelezaji wake, lakini  pia aliahidi  kuchukua maoni /ushauri wote na kuyawasilisha ngazi ya juu.” Mwisho wa kunukuu.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY; 

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa