• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA MADIWANI KUTOKA IRINGA MC WATEMBELEA MACHINJIO YA KISASA SONGEA MC

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2023

Manispaa ya Songea imeendelea kupokea wageni kutoka nje Mkoa wa Ruvuma wakifika katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika utekelezaji na usimamizi wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kwa mara nyingine tarehe 22 Mei 2023 Manispaa ya Songea ilipokea  Waheshimiwa Madiwani kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ambao  walikuja kwa lengo la kujifunza namna inavyoendeshwa na kusimamia machinjio ya kisasa ya Songea ikiwemo na tozo, na kiutawala.

Akizungumza Mstahiki Meya Manispaa ya Iringa  Ibrahimu Ngwada alisema Manispaa ya Iringa ina machinjio ambayo bado haijakamilka japokuwa imeanza kufanya kazi na huchinja katika mfumo ambao sio wa kisasa.

Mhe. Ngwada alisema kupitia hilo walipendekeza kuja Manispaa ya Songea ili kuboresha utendaji wa kazi pia kuendelea kuweka  mahusiano ya ki-Halmashauri hasa  ikiwa  inaendesha miradi inayofanana ni muhimu ujifunze kupitia  wengine.

Kwa upande wake Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano aliwakaribisha wageni hao na kisha kuwaongoza katika kila hatua ya uendeshaji wa mradi wa Mchinjio  ya kisasa iliyopo kata ya Tanga Manispaa ya Songea.

Naye Mkurugenzi Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alianza kwa kuwakaribisha wageni kisha alieleza Mradi huo umegharimu kiasi cha Bil. 5.7 na umeanza kutoa huduma japokuwa bado haujakamilika kwa asilimia 100%.

Alisema kuwa mfumo wa uchinjaji nyama katika machinjio hiyo ni wa kisasa ambao unatumia mtambo ambapo Manispaa ya Songea ni miongoni mwa miji michache nchini Tanzania ambayo inatumia mtambo huo.

Dkt. Sagamiko aliongeza kuwa kupitia machinjio ya kisasa mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea yameongezeka  ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 walikisia kukusanya kiasi cha Mil 379.

Kwa upande wa waheshimiwa Madiwani walisema wamejifunza mambo mengi kupitia ziara yao na kujifunza namna mtambo wa kisasa  unavyofanya kazi, miundombinu, sambamba na uwepo wa kichomeo cha wanyama  ambao hawafai kwa kuliwa na mwanadamu. “Walishukuru”

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa