• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA AFYA, JINSIA, WANAWAKE, WAZEE NA WATOTO AHAMASISHA CHANJO MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: August 12th, 2021

NA; “Amina Pilly.”

 

Naibu Waziri wa Afya, Jinsia, Wanawake, Wazee na Watoto Dkt. Mwanaidi  Hamisi anaendelea na  Ziara  Mkoani   Ruvuma  ambapo ataweza kutembelea  chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale, Hospitali ya Mkoa Songea (HOMSO) na Halmashauri nyingine kwa ajili ya kufanya uhamasishaji wa wazee ili waweze  kujitokeza kupata chanjo ya kujikinga na maambukizi ya UVIKO 19.

Dkt. Mwanaidi   alisema hayo akiwa  katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma jana 11 Agost 2021 kwa lengo la kukagua utekelezaji wa shughuli za Wazee na ustawi wa Jamii ikiwa ni sehemu ya  utekelezaji wa Sera ya Mkakati wa Maendeleo ya jamii ya 1996,  Wanawake na jinsia  ya mwaka 2000 na Sera ya maendeleo ya mtoto ya mwaka 2008, Sera ya Taifa  ya mashirika yasiyo ya Kiserikali 2001 na Sera ya Wazee 2003.

Miongoni mwa maeneo aliyoweza kutembelea ni pamoja na Hospitali ya Mkoa ambapo aliweza kukagua Chumba  maalumu kwa ajili ya matibabu kwa wazee, Chumba maalumu kwa ajili ya Chanjo ya UVIKO 19, kisha kuchomwa chanjo hiyo kwa lengo la  kuhamasisha wakazi wa Mkoa wa Ruvuma pamoja na Wazee kuweza kujitokeza kwa wingi  kupata Chanjo hiyo, pia ametembelea Shirika lisilo la kiserikali ROA pamoja na kikundi cha wananwake  Malkia wa Nguvu kilichopo Kata ya Mjimwema ambapo alitoa zawadi ya rollu tano za kamba kwa ajili ya kutengenezea makapu ya kikundi hicho.

Dkt. Mwaaidi amepongeza Shirika la lisilo la kiserikali ROA kwa jitihada walizozionyesha za kuwafikia wasichana 3201  kwa kuwapatia elimu ya kupambana na unyanyasaji wa kijinsia, na kuimarisha ulinzi na ustawi kwa wananchi.

Amewataka wananchi Mkoani Ruvuma kuendelea kujikinga dhidi ya maambukizi ya UVIKO 19 kwa kunawa maji tiririka, kutumia vitakasa mikono, kuvaa barakoa, pamoja na kuepuka mikusanyiko isiyo na lazima.

Naye mwenyekiti wa ROA  Mathew C.N. Ngalimanayo alisema “ ROA ilianzishwa ili kushughulikia masuala ya ustawi na maendeleo ya makundi yaliyo katika hatari ya kuathrika/kuathiriwa na umaskini na magonjwa.

Ngalimanayo aliongeza kuwa dhamira ya ROA inalenga kubuni, kupanga na kutekeleza mipango inayolenga kuwafikia, kuwasaidia, kuwaokoa na kuwaendeleza watu walio katika hatari ya kuathirika/kuathiriwa na umaskini na magonjwa kwa kushirikiana na wananchi, Serikali na wadau wengine.

Miradi hiyo imeweza  kushughulikiwa katika maeneo makuu ambayo ni pamoja na  Kinga dhidi ya VVU/UKIMWI, Huduma za VVU/UKIMWI majumbani (CBHS), Unasihi na upimaji wa VVU/UKIMWI kwa hiari, Ukatili wa kijinsia, Kujenga uelewa kwa jamii kuhusu Uzazi wa  Mpango ambapo Mradi huo unatekelezwa katika Halmashauri tano za Mkoa wa Ruvuma ambazo ni (Songea MC, Songea DC, Mbinga TC, Mbinga DC na Nyasa DC).

Aliongeza kuwa mradi wa USAID Boresha Afya unatekelezwa kwa kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wengine wa maendeleo ambapo Shirika la “Deloitte Tanzania” kwa mwaka 2020/2021 tumesaini mkataba wa Tshs. 890,000,000.00 ambapo kati ya fedha hizo Tshs. 10,260,000.00 ziliingizwa kwenye akaunti ya ROA na Tshs. 879,740,000.00 zinalipwa kutoka Ofisi ya Mfadhili moja kwa moja kwa walengwa.

Akibainisha changamoto zinazoikabili taasis hiyo ni pamoja na   Ukosefu wa fedha za kutosha za kuendesha shughuli za Shirika kadiri ya malengo yao, Ongezeko kubwa la walengwa wanaohitaji huduma  tofauti na rasilimali zliizopo, Kutofanikiwa kuwa na mradi wa moja kwa moja wa matunzo na misaada kwa Watoto yatima na Watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, Ugumu wa usimamiaji na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za mradi wa Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI unaofadhiliwa na “Deloitte Tanzania” kwa sababu ya utaratibu wa mfadhili kuhodhi kiasi kikubwa cha fedha.

Alisema Mradi umeweka mpango wa utekelezaji kwa kutoa misaada na matunzo kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, Kuwezesha Kiuchumi Familia zenye watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, Kujenga na kuimarisha uelewa kwa Jamii juu ya haki na wajibu wa watoto, Kushirikiana na Serikali na wadau wengine kuhakikisha wananchi wanakuwa na uelewa mpana juu ya masuala ya ukatili wa Kijinsia na Ukatili dhidi ya watoto.

AFISA HABARI - MANISPAA YA SONGEA.

12 AGOST 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa