Mtazame Afisa Maliasili na utalii wa Mkoa wa Ruvuma Africanus Challe anazungumzia vivutio vya kipekee na adimu ambavyo havipatikani sehemu nyingine yoyote Duniani zaidi ya hifadhi ya Gesimasoa iliyopo wilayani Songea mkoani Ruvuma . Hapa anazungumzia chanzo cha Mto Ruhuhu ambao upo kwenye hifadhi ya Gesimasoa ambapo kuna maingiliano ya mito Hanga na Lutukira inaunda mto Ruhuhu unaomwaga maji yake ziwa Nyasa.
MTAZAME Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Tina Sekambo akizungumzia maendeleo ya miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inatekelezwa katika Manispaa ya Songea ikiwemo inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ni ujenzi wa barabara za lami,ujenzi wa machinjio ya kisasa,ujenzi wa stendi ya mabasi ya kisasa na ujenzi wa bustani ya manispaa ya Songea.Pia Manispaa inatekeleza miradi mingine mingi ya maendeleo.
SHULE ya sekondari ya wavulana Songea (Songea Boys) iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imewekwa katika mpango wa kuletewa kiasi cha shilingi milioni 325 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa matano na mabweni matatu.Timu ya wataalam wa Manispaa ya Songea ikiongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo imetembelea shule ya sekondari ya wavulana Songea, eneo ambalo litajengwa madarasa matano na mabweni matatu.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa