WAUMINI wa Kanisa katoliki Parokia ya Ifinga Jimbo Kuu katoliki la Songea wamechangia zaidi ya shilingi milioni saba kwa ajili ya ukarabati wa kanisa la parokia hiyo ambalo linahitaji zaidi ya shilingi milioni 68 kufanikisha ukarabati huo.Akitangaza fedha zilizopatikana katika harambee iliyofanyika katika kanisa la Mtakaifu Galus Ifinga,mgeni rasmi Mbunge wa Jimbo la Madaba ambaye aliwakilishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Madaba Vestus Mfikwa,alisema kati ya fedha hizo pesa taslimu ni shilingi milioni 3.39 na ahadi ni shilingi milioni 3.6.Kanisa katoliki la Mtakatifu Galus Parokia ya Ifinga Jimbo Kuu katoliki la Songea lilijengwa na wamisionari wa kijerumani mwaka 1932 hivi sasa lina miaka zaidi ya 90. Kanisa hili kongwe nchini linahitaji ukarabati kwa sababu hivi sasa baadhi ya kuta zake zimeweka nyufa pia linavuja hivyo linahitaji ukarabati mkubwa ili kuliokoa lisianguke.Paroko wa Parokia ya Ifinga Padre John Otete anawaalika watu wote wanauguswa kusaidiana na waumini wa Ifinga kuchangia ukarabati wa kanisa hili.Paroko anawaalika watu wote waliopo ndani na nje ya nchi kuchangia ukarabati wa kanisa hili iwe kwa fedha taslimu au vifaa.Makadirio ya ukarabati ni fedha za kitanzania shilingi milioni 68.Unaweza kuchangia kupitia akaunti ya Benki au Simu kama ifuatavyo:1.JINA LA AKAUNTI:PAROKIA YA MTAKATIFU GALUS IFINGAJINA LA BENKI:NMB TAWI LA SONGEANAMBA YA AKAUNTI:618100352662.MWENYEKITI WA KAMATI UCHUMI NA UJENZI PAROKIA YA IFINGA MR.KINEMO KIHOMANOMPESA 07543349343.MHASIBU MR.GEBHARD NYONIMPESA 07540231154.PAROKO WA PAROKIA YA IFINGA PADRE JOHN OTETEMPESA 0756313380KUTOA NI MOYO,CHANGIA KAZI YA MUNGU,WOTE MNAKARIBISHWA.
MWENYEKITI wa Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma Vestus Mfikwa amewaahidi wakazi wa kijiji cha Ifinga kuwa serikali katika mwaka mpya wa fedha wa 2018/2019 imetenga bajeti ya kutosha kuhakikisha kuwa sehemu korofi katika barabara hizo zinafanyiwa matengenezo makubwa .Amesema kijiji hicho pia kitafungukiwa huduma ya mawasiliano ya simu na kwamba hivi sasa mikataba dhidi ya kampuni ya simu ya hoteli imesainiwa na baada ya mwezi mmoja mkandarasi anatarajia kuanza kujenga mnara wa simu katika kijiji hicho.Kijiji cha Ifinga kinakabiliwa na changamoto ya kukosa miundombunu bora ya barabara hali ambayo inasababisha wananchi kulipia shilingi kati ya 40,000 hadi 70 kusafiri umbali wa kilometa 48.Kijiji hicho pia hakina mawasiliano ya simu.
PAROKO wa Parokia ya Ifinga Jimbo Kuu Katoliki la Songea Padre John Otete amesema kitendo cha jumuiya ya waumini wa parokia hiyo kuchangia shilingi milioni saba kwa ajili ya ukarabati wa kanisa hilo kumejenga na kufungua ukurasa mpya na hivyo kuachana na mawezo tegemezi ya kuwasaidia wahisani toka nje ya nchi kuwajengea makanisa.Kanisa katoliki la Mtakatifu Galus Parokia ya Ifinga Jimbo Kuu katoliki la Songea lilijengwa na wamisionari wa kijerumani mwaka 1932 hivi sasa lina miaka zaidi ya 90. Kanisa hili kongwe nchini linahitaji ukarabati kwa sababu hivi sasa baadhi ya kuta zake zimeweka nyufa pia linavuja hivyo linahitaji ukarabati mkubwa ili kuliokoa lisianguke.Paroko wa Parokia ya Ifinga Padre John Otete anawaalika watu wote wanauguswa kusaidiana na waumini wa Ifinga kuchangia ukarabati wa kanisa hili.Paroko anawaalika watu wote waliopo ndani na nje ya nchi kuchangia ukarabati wa kanisa hili iwe kwa fedha taslimu au vifaa.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa