AFISA Utumishi Mkuu wa Manispaa ya Songea mkoani RUVUMA Lewis Mnyambwa amewatahadharisha watumishi wapya kuwa makini na mikopo inayotolewa na baadhi ya Taasisi za fedha badala yake amewashauri kukopa katika Taasisi za serikali kama Benki ya NMB ambayo mishahara ya watumishi wengi inapitia huko. Mnyambwa alikuwa anazungumza katika Kikao kazi cha watumishi wapya zaidi ya 100 ambao wameajiriwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuanzia mwaka wa fedha wa 2016/2017.Katika kikao hicho mada mbalimbali zimefundishwa zikiwemo kanuni za maadili ya utendaji katika Utumishi wa umma,HAKI,wajibu na stahili za watumishi wa umma,mfumo wa upimaji wa utendaji kazi katika Utumishi wa umma na mwongozo wa mavazi katika Utumishi wa umma.
Mkuu wa Majeshi Tanzania Venance Mabeyo amesema zoezi la kukinasua Kivuko cha Mv. Nyerere limefikia pazuri tayari wamekiinua upande mmoja.
MTAZAME Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na watumishi wa mkoa huo wakiwemo walimu ambapo amekemea tabia ya baadhi ya maafisa watumishi na wakuu wa Idara kusababisha watumishi waliopo chini yao kutopandishwa madaraja kwa uzembe wao hali ambayo inasababisha watumishi walioanza kazi mwaka mmoja kutofautiana katika ngazi za mshahara.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa