MASALIA ya mijusi mitatu iliyoishi miaka milioni 240 yamegundulika katika Hifadhi ya Litumbandyosi Bonde la Ruhuhu mkoani Ruvuma.Ugunduzi huo unaufanya mkoa wa Ruvuma kuwa na aina Mpya ya utalii
MRADI wa ujenzi wa chuo cha Ufundi Stadi VETA Namtumbo mkoani Ruvuma kilichogharimu zaidi ya shilingi bilioni 6.32 umekamilika.Mwakilishi wa VETA na Mkuu wa Chuo cha VETA Songea Gideon Ole Lairumbe amesema majengo yamekabidhiwa VETA na Mwezi ujao vifaa vya Ufundi vinaanza kulelea. na kwamba chuo hicho kitahudumia mikoa yote ya kusini
Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa tisa nchini ambayo imeweza kuwapeleka katika kidato cha kwanza Januari 2019 wanafunzi wote waliofaulu darasa la saba 2018.Waziri katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Seleman Jaffo amesema Wizara imekamilisha zoezi la uchaguzi wa Wanafunzi wa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2019 ambapo jumla ya wanafunzi 599,356 sawa na asilimia 81.76 kati ya 733,103 waliofaulu wamechaguliwa.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa