MMOJA wa wanamuziki wa kizazi kipya katika Manispaa ya Songea ZM akitumbuiza kwenye kampeni za Furaha Yangu ngazi ya Mkoa wa Ruvuma ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais ambaye aliwakilishwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.
Rais Magufuli amekemea vitendo vya uvuvi haramu katika Ziwa Victoria huku akiunga mkono jitihada ambazo zimekuwa zikifanywa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina katika kukabiliana na tatizo hilo. Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye viwanja vya Ukuta mmoja Mjini Nansio, wilayani Ukerewe, Rais Magufuli ameeleza kwa kina madhara ya uvuvi huo huku afichua kuhusu kilichofanya meli ya uvuvi iliyowahi kukamatwa katika Bahari ya Hindi, izame.
CHUO pekee kinachotoa mafunzo ya Ufamasia katika ukanda wa Kusini kimeanzishwa katika Kata ya Msamala Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.Mkurugenzi wa Kampuni ya TOPONE LIMITED ambao ndiyo wamiliki wa Chuo hicho Pascal Msigwa amesema chuo hicho kinatarajia kufunguliwa Oktoba mwaka huu ambacho kwa kuanzia kitakuwa kinatoa mafunzo ngazi ya cheti ambayo yanachukua miaka miwili.Msigwa amesema chuo hicho kimesajiriwa na Baraza la Ufundi la Taifa (NACTE) na kupewa namba ya usajiri 184 na kwamba lengo la kuanzisha chuo hicho kuiunga mkono serikali ya
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa