NAIBU Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Josephat Kandege yupo mkoani Ruvuma katika ziara kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo,akiwa katika Manispaa ya Songea ameikagua barabara ya Tumbani eneo la majengo Kandege amemwagiza Mkandarasi kuhakikisha kuwa barabara hiyo inawekwa lami nzito kabla ya mvua za masika hazijaanza Novemba mwaka huu kwa kuwa mvua zikiianza inakuwa ni kazi ngumu kuweka lami hivyo amewaagiza kuongeza kasi ili kusiwepo na kisingizio cha mvua.
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Josephat Sinkamba Kandege yupo mkoani Ruvuma ambapo anatembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.Naibu Waziri huyo wa TAMISEMI amekagua mradi wa ujenzi wa machinjio ya kisasa katika Kata ya Tanga manispaa ya Songea.Mradi huo ambao umefikia Zaidi ya asilimia 60 unatarajia kukamilika Oktoba mwaka huu ambapo hadi sasa Mkandarasi ameshalipwa Zaidi milioni 900 ambayo ni asilimia 35 ya malipo ya mradi huo ambao unagharimu Zaidi ya bilioni 3.2.
MRADI wa machinjio ya kisasa ya Songea umefikia Zaidi ya asilimia 60 unatarajia kukamilika Oktoba mwaka huu ambapo hadi sasa Mkandarasi ameshalipwa Zaidi milioni 900 ambayo ni asilimia 35 ya malipo ya mradi huo ambao unagharimu Zaidi ya bilioni 3.2.Akitoa taarifa ya mradi huo,Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Manispaa ya Songea Mhandisi Nicolus Danda amesema mradi wa machinjio ya kisasa unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya shilingi bilioni 3.2.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa