HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Septemba 13,2018 imesaini mikataba minne ukiwemo mkataba wa uendeshaji wa Bustani ya Manspaa ya Songea ambao umesainiwa baina ya Halmashauri ya Manispaa na Mwendeshaji aliyeshinda zabuni anayeitwa Neema Kajange.Hafla ya kusaini mikataba hiyo imefanyika katika ofisi ya Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassani Mshaweji mbele ya wanahabari.Mkataba wa uendeshaji wa bustani ya Manispaa ya Songea ni wa shilingi milioni 15 ambao utafanyika katika kipindi cha miezi kumi ambapo Mwekezaji ataendesha shughuli mbalimbali ikiwemo hoteli,choo na mchezo wa bembea.
Inakadiriwa homa ya ini inaua watu zaidi ya Milioni moja kwa mwaka kulingana na WHO. Wizara ya afya imetilia mkazo juu ya kujitokeza kupima na kufanya chanjo ya homa hiyo.Inakadiriwa kuwa watu milioni 240 kote duniani wana kirusi cha Hepatitis B, idadi kubwa ya maambukizi ikipatikana bara Afrika na Asia.
AWAMU ya pili ya mgawo wa pikipiki 10 kati ya 21 zilizotolewa kwa Waratibu Elimu 21 wa kata 21 zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma zimekabidhiwa leo katika viwanja vya ofisi ya Manispaa ya Songea.Waratibu Elimu Kata 11 tayari walikabidhiwa pikipiki 11 katika awamu ya kwanza.Pikipiki hizo zimetolewa kwa waratibu elimu kata 2894 katika nchi nzima lengo likiwa ni kuzitumia kusimamia maendeleo ya elimu katika kata zao.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa