jivunie Mbunda ni mwanamume mwenye ulemavu. Amemuoa Bahati Ramadhani tangu Mei mwaka 2018. Hatahivyo kabla ya kupata upendo na furaha hii - anakiri haikuwa rahisi kwani aliwahi kukataliwa na wachumba 15 kutokana na ulemavu wake.Mchumba wa 16 ndiye alimkubali.
Mji wa Liwale uliopo katika Mkoa wa Lindi Mei 13 mwaka huu ulizizima kwa nderemo na vifijo kwa muda wa saa sita baada ya Mlemavu Jivunie Mbunda mwenye umri wa miaka 35 kufunga ndoa na Bahati Ramadhani mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa Newala mkoani Mtwara.
Mbunda akiwa na mkewe Juni mwaka huu alitembelea Bunge ambao kwa pamoja wabunge zaidi ya 300 kila mmoja alimchangia Mbunda shilingi 20,000.
MTAZAME Waziri wa Maliasili na Utalii Dk.Hamis Kigwangalla alipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyopo mkoani Kigoma
Wananchi wa Tanzania na Afrika Mashariki wapo katika hatari ya kupata maambukizi ya Homa ya Ini, hususan aina ya B na C, kutokana na kuwa njia za maambukizi ya Virusi hivi hufanana na zile za maambukizi ya VVU.Hapa Tanzania, takwimu kutokana na tafiti chache zilizopo zinaonesha uwepo wa maambukizi ya virusi vya Homa ya Ini aina ya B na C. Mfano, kati ya wachangiaji damu 200,000 kwa mwaka 2016, asilimia 6(takriban watu 12,000) walikuwa na maambukizi ya Homa ya Ini aina ya B.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa