NAIBU Waziri wa Madini Doto Biteko amefanya ziara katika machimbo ya Ngapa yaliyopo wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma na kuzungumza na wachimbaji wadogo wanaochimba madini ya vito aina ya Gem Stone na kubaini wachimbaji wadogo wananyonywa na wafanyabiashara katika hali inayosikitisha. Imebainika kuwa baadhi ya wafanyabiashara wananunua madini hayo kwa bei ya chini ambapo wao wanakwenda kuyauza madini hayo mara 15 ya bei walionunulia.Wilaya ya Tunduru haijanufaika na madini tangu mwaka 1996,ambapo kwa mara ya kwanza imepata mapato ya madini katika mwaka 2017/2018 kwa kupata shilingi milioni 66,baada ya ya serikali kurekebisha sheria ya madini ambayo inamwezesha mtanzania kumiliki madini.
MTAZAME Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akitoa maagizo mazito kwa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwenye kikao maalum cha kujibu hoja za ukaguzi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.
Pamoja na mambo mengine Mkuu wa Mkoa ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuweza kupata Hati inayoridhisha mara mbili mfululizo na kusisitiza kuwa mafanikio hayo yasiwafanye wakajisahau kwa kuwa ukaguzi wa mahesabu unafanyika kila mwaka hivyo kujiandaa na ukaguzi ujao kwa kupunguza hoja.
Naibu Waziri wa Madini Mhe.Doto Biteko ameutaka uongozi wa kampuni ya TANCOAL inayochimba madini ya makaa ya mawe katika machimbo ya Ngaka yaliyopo wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma kufanya kazi kwa kufuata sheria
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa