Mkuu wa wilaya ya Songea pololet Mgema amewaagiza wenyeviti wa serikali za mitaa katika Manispaa ya songea kuimarisha ulinzi na Usalama kuanzia ngazi ya mitaa.Mgema ametoa agizo hilo wakati anazungumza kwenye kikao ambacho pia kilishirikisha Kamati ya ulinzi na Usalama wilaya ya Songea,Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea na maafisa watendaji wote wa mitaa 95 na kata 21 za Manispaa ya Songea.
Mtazame mkurugenzi wa Saint Teresa Orphans Foundation (STOF)Teresa Nyirenda akizungumzia sababu zilizosababisha kuanzisha Shirika hilo na mafanikio ambayo yamepatikana tangu kuanzishwa kwake miaka 17 iliyopita.
Taasisi ya STOF ambayo inafanyakazi nchini Tanzania na Marekani inatarajia kufungua shule ya msingi ya kimataifa Januari mwaka 2020 katika eneo la Unangwa Kata ya SeedFarm Manispaa ya songea mkoani Ruvuma
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa