MKUU wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema amekabidhi msaada wa magodoro,vitanda na mashuka nyenye thamani ya shilingi milioni tano ambavyo vimetolewa na Benki ya NMB katika Kituo cha Afya Madaba kilichopo katika Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.
WANANCHI wa Kata ya Lilambo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wanatarajia kunufaika na mradi wa maji ya mtiririko wenye thamani ya shilingi bilioni 1.1,mradi ambao unatarajia kukamilika Juni 30,2019.
VIPIMO vya maabara vya mkemia mkuu vinaonesha kuwa kiwango cha sumu ya zebaki katika bandari ya Ndumbi ziwa Nyasa mkoani Ruvuma kimezidi mara tatu ya kiwango cha kawaida hali ambayo inatishia maisha ya watu na viumbehai vya majini.Akitoa ripoti ya ukaguzi kwa wataalam wa maji na mazingira wa Mkoa wa Ruvuma,kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea ,Mratibu wa Baraza la Taifa la Kudhibiti Mazingira(NEMC) Kanda ya Kusini, Lewis Nzali amesema vipimo vya kikemia vilivyochukuliwa katika bandari ya Ndumbi vinaonesha kuwa sumu ya zebaki imefikia 0.018Hg wakati kiwango kinachotakiwa ni 0.005Hg
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa