MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ametoa ametoa maagizo na maekezo kwa watendaji wa Halmashauri zote za mkoa wa Ruvuma.Ametoa maagizo hayo wakati anatoa Taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015 kipindi cha Julai, 2017 hadi Juni ,2018 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea.Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho,Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Profesa Riziki Shemdoe,Wakuu wa Wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma,watalaam ngazi ya Mkoa,viongozi na wajumbe mbalimbali wa CCM Mkoa wa Ruvuma
TAZAMA yaliyojiri katika ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa nchini China
Diwani wa Kata ya Majimaji Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Simbili Abdalah Makanyaga anazungumzia ongezeko la tembo katika Pori la Akiba la Selous linavyoathiri wananchi wa Kata yake.Kama tunavyofahamu kuwa wilaya ya Tunduru imezungukwa na pori la selous.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na utalii Meja Generali Gaudance Milanzi alipotembelea Pori la Selous Kanda ya Likuyuseka wilayani Namtumbo alisema serikali imedhibiti vitendo vya ujangili dhidi ya tembo hali ambayo imesababisha tembo kuongezeka kwa kasi na kuleta changamoto kwa wananchi wanaoishi jirani na hifadhi na mapori ya wanyamapori
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa